Ngonjera: Kubali Tu
KUBAKI TU
Inawezekana
ni mwenye usiri juu ya mabaya anayokufanyia mwenza wako.
Lakini, bado ndugu, jamaa, marafiki wakawa
wanajuwa kila kitu kuhusu yeye
na,
si ajabu wasikusaidie kwakuwa hawapendi uwe ni mwenye furaha kama wao au hata
kuwazidi. zaidi wanapenda huzuni na majonzi yatawale moyoni mwako
fikiria,
ikiwa rafiki yako ndiye msaliti utafanyaje? Ikiwa ndugu yako au boss wako ndiye
chanzo cha maumivu hayo utafanyaje?
Usishangae
wewe kuachwa au kuacha bali jiulize ni wapi unateleza hadi hayo yote yakukute ,
mhhhhhh… hata hivyo hakuna upendo unaodumu kwa kipimo kilekile cha awali.
Kubali
tu….. ,
Kubali
tu kuwa huyo so wako tena
Kubali
tu kuwa huyo so yule wa kipindi kile , Kipindi kile cha ua changa , ua ambalo
likifurahia kuchomoza kwa jua basi
lilifurahia pia kuzama kwake
Mmmmhhhhh
….. aaaaaaa haaaaa haaaaaaa.
Labda
pengine unajiuliza je, utawezaje kuishi
bila yeye….
Maana
kila ukitafakari unakosa majibu…..
Huenda
mtu huyo ni baba wa watoto wako
Huenda
mtu huyo ni mama wa watoto wako
Au
huenda mtu huyo ni chanzo cha mafanikio yako.
Sikia, fumbua macho….
Amka….,
fikiria
kwa kina, ikiwa wewe umeweza kuwa na
hofu dhidi ya wema wake au umuhimu wake kwako.
je yeye alishindwaje kuujuwa umuhimu wako …
alishindwaje
kuijua thamani yakooooo…. (kwa ukali)
Eti…? alishindwaje kuutunza uaminifu wenu na hata
akadiliki kukufanyia machafu anayokufanyia.
Ni
mara ngapi amekuwa akirudia makosa yale yale kila mara ulipo msamehe.
Kwanini
usimsahau.
Harafu….
Inashangaza
sana, yaani kama unaweza kumsahau marehemu ilihali alikutoka ikiwa unamuhitaji,
wakati anakuhitaji, ilihali wewe au yeye hakuna alojuwa ni nani atamtangulia
mwenzie lakini bado uliweza kumsahau…..
Na
je, vipi kuhusu huyo uliyemfumania mara kadhaa
Au
Vipi huyo anayekuongopea kila siku…. au Mtu anayekupotezea muda wako , nguvu
zako, mambo yako mengi yameharibika kisa yeye.
Unasindwaje
kumsahau…
Mhh
Mtu ambaye mmekutana tu ukubwani.
Tatizo
hapa so kupigania penzi au kumpigania mtu bali cha muhimu hapa ni kuipigania
furaha yako.
Huwezi
kuwa na furaha wakati huna amani.
Na
hauwezi kuwa na amani wakati uliyenaye si mwaminifu.
Na
wala usije kujiaminisha kuwa raha za kimwili ni bora zaidi kuliko amani ya moyo
.
Amka
toka usingizini
Kubali
kuwa huyo so type yako tena
Afu
kwa kifupi hakuna kitu kisichopokea mabadiliko kamwe….
Kila
kitu huanza na huisha pia.
Amini
tu kuwa upendo wenu umefika mwisho kabla ya kifo kuwatenganisha.
Nikukumbushe
tu kuwa hiyo ndoa yenu au uchumba wenu
wa muda, isiwe sababu kwenu kushikilia yalopita, eti yanakufurahisha kila
uyakumbukapo. Hapana… huo ni ujinga.
Kumbuka, ndoa ni sheria tu iliyowekwa kulinda
mahusiano ya watu wanaopendana au mtu aliyependa hata kama yeye hajapendwa.
Harafu…. Ndoa si ishara tosha ya upendo ama kujuwa kuwa watu fulani
wanapendana…. Bali, ni kifungo tu kama
vifungo vingine. Vifungo ambavyo hata wasio na hatia hujikuta wakifungwa…
Wala
Ndoa haiwezi kukupa uhuru wala nafasi ya kufanya marekebisho juu ya usahihi wa chaguo lako
Huwenda uliyenaye si chaguo sahihi kwako….
Je,
Utafanya nini ikiwa uliye naye sasa si mwaminifu….
Etiii….
sema….
Utafanya
nini…
Basi
labda nikusaidie kujibu…
Muache……
Tena
asirudi kwenye maisha yako kamwe…..
Ikiwa
unaweza kuishi bila wale ulowapenda kabla na hata ukayatoa maisha yako kwaajili
yao kabla ya wao kufariki. Je,
unashindwaje kuishi bila huyo msaliti, tapeli, jambazi , tena mnafiki , mtu
asiyeitambua thamani yako
Achana
naye…
Narudia
kusema ….
Achana
naye…
”Hakufai
hata chembe mtu huyo”…
Naomba
nimalize kwa kusema haya….
Siku
zote upendo hutengenezwa
Kwa
maana hiyo Upendo huzaliwa, hukuwa huishi
na hata kufa.
‘TUJIFUNZE KUSAHAU’’ ILI MAISHA MAPYA YAENDELEE
Maoni