Shairi: Kipenzi changu
Halooo…
Halooo…
Chozi hili lanibugujika,
Ni kwasababu
nimekukumbuka,
Sakura
aaaa….. mamaa afriaka,
Si kwa
ukimya huo,
unanifanya
niumie mwenzio,
Sakuraa wewe
ndo langu kimbilio,
Kwa mwingine
sioni singizio.
Nimeyafunga
yangu macho,
Ili tu
nisitamani vipitacho,
Hakuna
kinitesacho,
zaidi ya penzi lako,
Hakika ndani
ya huu moyo,
uko peke
yako.
Sakura
kipenzi…
Naomba
nivumilie kwa kipindi hiki,
Nyakati
iliyojaa shida na dhiki,
ukidhani
siwakumbuki,
Au pengine
nadhihaki
Mama afriki.
Kila siku
napiga goti chini,
nikinyoosha
mikono yangu juu,
nikikuombea
furaha na amani,
nikiomba
mungu aulinde upendo huu.
Najuwa pesa
ndo kimbilio la kila mtu,
Ila
tafadhari usije niacha peke yangu,
Ukawafuata
wenye vitu,
Ukaniacha
mimi kapuku nikilia kwa machungu.
Najuwa mbali
nipo,
Hasa na upeo
wa mboni za yako macho,
Ila tambua,
Popote ulipo
nami nipo,
Mfano wa
giza na popo.
Kuna wakati
namiss uwepo wako,
Kuna wakati
namiss penzi lako..
Ile michezo
yako…
Mideko na
yale malingo,
Tukiimba na
kurushiana mito,
Yaani kama
watoto.
Haikuwa tomato,
Haikuwa
avocado,
Bali ni
upendo,
Ndiyo unipao
haya mawazo.
Ikiwa umbali
ni sumu ya penzi,
Basi kuonana
ndo tiba pekee,
Ikiwa bila
wewe kuishi siwezi,
Basi penzi
langu niwekee.
Na kama
kupenda ni uchizi,
Basi acheni
nipotee,
Lakini
kukuacha siwezi,
Amini wewe
ndo wangu wa pekee.
Najuwa
utakuwa na hasira,
Najuwa
unahitaji hela,
Naelewa
huwezi lala bila kula,
Najuwa
umechoshwa na huu ufukara.
Naelewa kuna
time unajiona fara,
Na vile sina
ajira,
Unahisi
umepata hasara,
Unahisi umepoteza
dira.
Naomba
mpenzi tafadhari,
Penzi letu
usije liweka kando,
Naomba kwa
hili jihadhari,
Afriq wangu
mfunze upendo.
Kamwe usiwe
mbali,
Mfunze
kuhusu uzalendo,
Sitopenda
awe na kiburi,
Naomba
ichunge mienendo.
Tena
lisimamie hili,
Asifiwe kwa
uzuri wa matendo,
Muandae kuwa
na akili,
Hakikisha
anacheza nawe kando,
Muweke mbali na michezo ya magendo.
na Kilimboka
Maoni