Shairi : Chini Ya Jua
Chini ya jua
Kunawatu
wanaishi kwa kutegemea dhiki za watu…
Kwao utu si
kitu
Kwao pesa
ndo kila kitu.
Ni chini ya
jua….
Mengi
utayatambua
Huko hakuna
siri kila kitu ni dhahili..
Chini ya
jua….
Huku ukitaka
kumjua asiyekupenda
Basi patwa
na shida…
Chini ya jua
Kuna viumbe
hupenda kuishi kuliko kufa
Uzushi
kuliko taarifa
Raha kuliko
tabu….
Chungu
kuliko tamu
Huko chini
ya jua
Vya haramu
ndivyo vinaumuhimu….
Chini ya jua
Watu
wanapenda uzinzi kuliko kazi…
Watoto wa
nje ni wengi kuliko wa ndani.
Akiba ni
ndogo kuliko madeni.
Chini ya jua
rushwa ni
bora kuliko kula
Huku wengi
huamini sana kulogwa kuliko kugongewa
Wengi wao ni
wazawa waliojiweka utawa
Huona raha
wakisifiwa
Hawaoni
ajabu wakidaiwa.
Chini ya
jua…
Kuna viumbe
wa ajabu sana
Hawa aibu
hawana..
Wao kwa wao
huchapana
Mikia
kulishana
Nyonga
kushikana
Hawachelewi
mapajani kuwekana.
Chini ya
jua.
Litokealo
lea afadhari ya jana.
Chini ya jua
Huko bhana
ndoa so kikwazo
Eti
utaondosha mawazo
Huko ndoa ni
likizo
Tena pango
la kuficha uozo
Kimbilio
pekee la watu waroho na waongo.
Chini ya jua
Kuna viumbe
wanaimani kuliko hata wanaye muamini….
Huku kuna
viumbe wanaogopwa kuzidi hata maanani.
Chini ya jua
Kuna people
Hawana kazi lakini wanalipwa..
Hawana hadhi
lakini wanalindwa
Hawana mioyo
lakini bado wanapendwa
Daaaaaa…
Wao
kucheka hadi wakuone ukilia
Wao kununa
hadi wakuone ukiendelea.
Huko chini
ya jua…
Kuacha
kuachwa ni jambo la kawaida…
Wanaamini
hakuna danga lisilo na faida
Wala buzi
lisilochunika….
Huko ukila
nawe juwa umelika
Ukilia
usitarajie kucheka
Ukipenda
jiandae kuachika
Na kama
ukipendwa basi jiandae kutajirika.
Huko chini
ya jua
Kuna nishati
lakini hawana mwanga….
Asubuhi
jua mchana majanga
Mchana dua
jioni kipenga.
Huko chini
ya jua
Kuna visoke
wabeba unga
Kuna makundi
ya wanga kuliko waganga
Mabibi
washika nyanga, mafundi wa kuchezea anga.
Chini ya jua
Huko walinzi
hawajui kupiga kipenga
Zaidi wa
migambo kushika mapanga
Kusumbua
wanaopanga.
Wenye nyumba
walojenga.
Huko chini
ya jua
Wanamaisha
ya ajabu sana
Yaani wana
vyanzo vya maji
Lakini nguvu
ya kuoga hawana
Wanamifereji
lakini ndoo hawakingi
Wanachemchem
lakini misingi hawajengi
Hawana
kiu wanaokufa ni wengi.
Huko chini
ya jua.
Kuna wasomi
wengi kupindukia
Wasio na
haki wasio na hatia
tena ni
wachache walio na njia
Wengi wao
hawajui wapi pakuanzia.
Chini ya jua
Huko hakuna
kigeni
Wala habari
ya amani
Huko mauaji
ni hadharani
Si ya dereva
wala hayawani
Milipuko ya
vimondo na volkani.
Huko chini
ya jua
Kila mtu
anataka usikani
Nae aingie
barabarabarani
Huko chini
ya jua
Eti
ukijifanya unajua
So ajabu
wakakwanua
‘’CHINI YA JUA’’
na Kilimboka
Maoni