Shairi: Nakupenda

 

Nakupenda

Kwa urembo ulionao sijawahi kukutana nao

Maana kila napopita nakutana na story zako

Wewe ni mrembo…….

 

Kama kupenda ni kosa basi wewe ndiye unayestahili hukumu hii….

Maana Si mimi chanzo bali ni huo uzuri wako…

 

Jiulize…

…. Ni marangapi nimekuwa nikiteseka ili kukupata wewe.

Na  leo hii umekuwa wangu.

 

Do You know why wakati  flani nakuwa mkali

Coz..

Naogopa kuchanganywa..

Naogopa sana kuibiwa….

Mwenzio naoogopa kuumizwa

 

Mpenzi wangu nakupenda sana.

 

Naaaa …. kila siku kwangu ni maalumu na muhimu  Hasa napokuwa na wewe…

Wewe ni zaidi ya mwangaza wa jua…

Nuru iliyo na thamani kwa maisha ya viumbe

Nadhani hili unalitambua.

Hivyo pasina wewe mimi si kitu hapa duniani

 

laazizi…

Kuna wakati huwa najiuliza kwanini  unafeet kwenye vazi la kila rangi

Basi nimekuja kugundua kuwa ni kwa sababu nakupenda sana.

Ni upofu wa aina gani huu nisiweze hata kukutoa kasoro juu ya huo uzuri wako.

Kiumbe uliyehumbika  kwa rangi na sura

hakika wewe ndiye yangu furaha.

 

Tazama huo muondoko

Tazama hiyo mideko..

Pua na hiyo midomo..

Nani kama wewe au hata wa kukuzidi

Naimani hakuna….

Si kwa Ucheshi wako….

Ukalimu kwa ndugu zangu….

Na hata watu wanaotuzunguka

 

Mwandani wangu…

Uhai wangu ni wewe….

Furaha yangu ni wewe…

Wewe ndo kila kitu kwangu

Nakili kwa kinywa kuwa nimeumbwa kukutumikia wewe…

Wewe ndo hatima yangu…

Kamwe sitokubali nikuache nyuma.

 

Kwa chozi lako nitalia

Kwa huzuni yako nitaumia pia

Kwenye hatali nitakukimbilia

kwa yeyote nitamshambulia

Na si furaha yako kukuharibia.

 

 

Hata hivyo..

Siwezi kuianza siku yangu mpya bila wewe

Bila kukuona

Bila kuisikia walau sauti yako.

 

Mahabuba….

Fundi wa haya mahaba

Kiumbe pekee mwenye kunilisha nikashiba

Usiye juwa roho wala iba

Ama kwa hakika moyo wangu umeubeba…….

 

Takuwa mnafiki nisipo kushukuru

Ahante kwa kunifanya kuwa huru

Asante kwa penzi hili lenye nuru

Asante kwa kunihepushia misururu

maisha ya kuishi kama kunguru

Na leo mimi si  waluwalu.


na Kilimboka

 

Maoni

Mashairi Pendwa Zaidi

Ushairi : Maumivu

Shairi: Kipenzi changu

Shairi: Moyo Wa Subira