Shairi: Moyo Wa Subira
Moyo wa subira
Subira
hurejesha furaha iliyopotea
Moyo
wenye subira daima hauwezi teketea.
Daima
ni wenye kukuwa na kuendelea
Moyo dhaifu hauachi kupendelea
Moyo
ulopenda ni kawaida kuumia
Ndiyo
maana hauchoki kuvumilia
Upendo
haujaribiwi kamwe
Wala
Penzi so shamba eti mwaka huu lisilimwe
Mapenzi
ni bustani ili itembelewe ipendwe
Ni
lazima isafishwe na itunzwe
Halafu
..
Kwenye
haya maisha wewe ni nani hadi usisemwe
Kwenye
mapenzi haya wewe ni nani hadi usiumizwe
Wewe
ni nani eti muda wote upendwe…
Usinyimwe….
Usiachwe…. usifiwe…
Kumbuka
So kila kitu kipo kwa ajili yako wewe.
Vingine
vina wenyewe
Wapo
lakini so kila mtu ataguswa nawe
Bali
upendo wa kweli huanza ndano yako mwenyewe
Na
Kwenye maisha yako usitegemee kupendwa na asokujuwa
Hivyo
wape nafasi wengine kukuelewa
Kwa
maana upendo wa kweli hutoka kwa wanaokutambuwa wakakuelewa.
Uaminifu
ni akiba yenye kuhitaji matunzo
Japo
upendo wa kweli huonekana mwanzo
Hata
hivyo
Penzi so pishi utake kionzo
Kwa
maana utamu wa chakula haushibishi tumbo
Chunga
sana usije kuwa chambo
Usije
sakamia mapenzi kwa kufuata mkumbo.
Moyo
ulokufa daima hausikii dawa
Na
siku zote ukikataliwa
Basi
tambuwa umechelewa
Na
kama siyo basi huenda mtu huyo hajakuelewa
Kwa
maana kupendwa nikubalikiwa
Kupendwa
ni kupendelewa
Kupendwa
ni kuaminiwa
Kupendwa
ni kukubaliwa
Hakuna
haja ya wewe kunung’unika
Eti
mtu furani amebadilika
Eti
mtu furani amekuchoka
Kwa
maana akupendaye hakika
Daima
atakushika
Huyo
ni wa kufa na kuzika
Unachokipenda
kamwe hakilingani na unachokitaka.
Kwa
maana upendo haupimwi kwa kushika
upendo
ni rangi isiyobadilika
Upendo
ni kumbukumbu isiyoweza kufutika
Hivyo
chunga usije ichoka
Kwa
maana upendo huja na kuondoka.
Upendo
ni amali inayohitajika kutunzika
Upendo
ni sawa na vita ipigwanayo bila kuchoka
Mapenzi
bahari
Ikiwa
safi ni mazuri
Ikiwa
chafu ni hatari
Mapenzi
ni kama chai
Ikikos
sukari haifai
Ikiwa
nayo utafurahi
Mapenzi
so kiu ya maji
Eti
ukiyapata imetosha
Wala
so bakuli la uji
Eti
ukipoa umekomesha
Na
mapenzi si vita ya miji
eti uipigane ikaisha
wala mapenzi so mtaji
eti
ukiupata basi umewin maisha.
Unaweza
kuipata ndoa na si furaha
Unaweza
usiwe na doa lakni ukawa na jeraha
Unaweza
kujikomboa lakini usiishi kwa raha
Unaweza
kumtoboa lakini usimtoe usaha
Siku
zote anaye kukomoa usimletee mzaha
Lengo
langu so kubomoa ila kutoa nasaha.
Maoni