Ngonjera: Ya Duniani
Ya duniani
Huwenda
hukuwa na utambuzi mzuri juu ya ile kauli isemayo kuwa uyaone.
Huenda
ni utoto tu na ujinga wa kipindi kile
ukiwa mdogo na ndiyo maana uliamini kuwa siku ukiwa mkubwa utakuwa na
maisha mazuri.
utakuwa
ni mtu maarufu sana, na utapendwa karibu na kila mtu,
utasaidia
kila mwenye uhitaji.
Na
kubwa kuliko utakuwa na mpenzi mzuri mwenye kumjali na hata mkawa ni watu wenye
kupendana sana.
Lakini
kumbe haiko hivyo….
Mambo
hubadilika siku hadi siku.
Na
hata hivyo haikuwa rahisi kwa wewe kuamua ni aina gani ya maisha uyaishi ili
hali wakati huo ulikuwa nimdogo sana na kwa bahati mbaya haukuwa na nafasi ya
kufanya maamuzi kwa wakati huo.
Zaidi
ulikuwa ni tegemezi kwa kila kitu kipindi chote cha makuzi yako hadi kufikia
sasa.
Na
sasa ni ni mtu mzima….
Unajuwa
baya ni lipi na lipi ni zuri….
Kwa
sababu hiyo, hatima ya maisha yako ya baadae huwa yapo mikononi mwa walezi
wako.
Hata
maisha unayoishi leo ni juhudi za walezi wako.
Iwe
ni kwenye mahusiano au hata katika shughuli za utafutaji bado walezi wako ndiyo
wenye kuashiria hatima ya maisha yako.
Maana
wao ndiyo wenye kukuandalia msingi wako wa maisha…
Hapa
niwape pole wale mlio na walezi ama wazazi wasiojitambua yaani vilaza…
Maana
mzazi mwenye kujielewa hawezi kushinda baa au kutwa akibadili wachumba, au mama
kutwa kubadili mitindo ya nywele na manukato ya bei ghali
ili
hali kizazi chake kinahangaika’’’
kinataabika…
mzazi
unashindania fashion za nguo, pikipiki,magari, namatoleo ya simu.
Na
wakati huo damu yake, mtoto wake, kijana
wake hana kazi hana mtaji wala hajui
afanye nini.
Kuna
wazazi, ni bora aweke bando la bukumbili
au tatu ili akeshe mtandaoni akichat lakini wakati huo mtoto wake hana vifaa
vya shule.
Huenda
wewe hapo unapitia magumu hayo kwa
sababu tu jana yako haikuwa nzuri…
Ndiyo…
jana yako haikuandaliwa vizuri na watangulizi wako.
Tazama….
leo hii mahusiano yako yanashida kwa sababu huwenda umekulia katika malezi ya
aina hiyo….
Baba
mama hugombana hadharani….
Ukiwa
mtoto huenda ulikuwa huku ukijuwa machafu ya tabia za wazazi wako.
Mtoto
mdogo kushirikishwa katika matukio kama usaliti, wizi, umbea , na hata uongo .
Lakini
haujachelewa….
Matendo
na tabia chafu zitaathiri maisha yako kwasababu ya uamuzi wako.
Uamuzi
utakaouchukuwa leo ili kuisahihisha kesho yako kutokana na makosa uliyokwisha
kufanyIka jana.
Chini
ya jua
akitakacho mwelevu kiwe, basi kinawezekana
kuwa
Hatufanikiwi
kwasababu tunawekeza katika kushindwa
wamefanikiwa
kwa sababu hapo kabla walianguka mara kadhaa… na waliwekeza katika kufanikiwa.
hivyo
mimi nawewe tunapaswa kupitia mchakato huo.
Mchakato
ambao huenda ukaghalimu hata uhai wako…
Kuna
kipindi utagombana na kila mtu…
Kipindi
hicho utapoteza kila ulichokipenda…
Kila
kitu kwako kitabaki kuwa historia…
Na
hapo ndipo utaanza kuingia katika majaribu ya hapa duniani.
Kama
ni chungu ya maisha basi hapa ndipo utaijuwa….
Na
hata ile kauli ya dunia duara basi hapa ndipo mahala pake…
Aisee
tujifunze kuyaheshimu na kuyazingatia maneno ya watangulizi wetu yaani wahenga.
Ama
kwa hakika wakati huo hutakaa ukausahau kamwe
Wakati
ambao utabaki kama msindikizaji tu wa mafanikio ya wenzako….
Utakuwa
na wakati mgumu kiasi cha kujichukia…
Wakati
ambao utapaswa kukubaliana na kila hali
Wakati
ambao utapitia kila aina ya shida…
Tabu
Maumivu
Dharau,
Lakini
huwezi amini hicho ndo kipindi cha mimi na wewe kuweza kusimama tena
Hicho
ndo kipindi cha wewe na mimi kurekebisha tulipokosea..
Kipindi ambacho kila kitu kitapaswa kuanza upya.
Uzima
ni zawadi ama ahadi isiyo na matumaini
ndani yake
Kwani
unaweza usiipate zawadi hiyo.
Na
kama ahadi hiyo itatimia basi kuna kila sababu ya kuwa watumiaji wazuri wa
ahadi hiyo.
Hivi
unatambua ya kuwa maisha haya bila wewe hayawezi kunoga…
Tena
kama ni chakula basi hakitakuwa na radha hata kidogo.
Raha
ya maisha uishi sambamba na wengine… uishi ukiona wengine wanaishi…. Wakuone
ukifurahia… uwaone wakifurahia pia.
Ukitembea
kama wao… ukilala kama wao… ukiamka kama wao… ukipumua kama wao…. Yaani wakuone
uwaone.
Na
ikitokea wewe uko na fura wao hawana hapo raha haitakuwepo…
Maana
furaha ya moyo hutegemea sana amani ya watu wakuzungukao.
Kwa
maana hiyo kasoro moja katika yote yaletayo uzima basi matokeo yake ni huzuni
na hapo maisha yako yatakuwa yameingiwa na dosari.
Maoni