Ushairi: Kwaheri Mama
Kwakheri mama
Ulipambana
hukupenda
kuniona
Eti
raha sina au nimenuna
Dear
mama…
Leo
Haupo nami tena
Kweli
Siwezi kukuona
Eeee
maulana
Ni
wewe mama uliyeshinda njaa
Ili
mwanao nipate kula
Ni
wewe mama uliyejinyima kuvaa
Ili
mwanao nipate pakulala
mama wewe ni shujaa
uliyekubali
hasara
uliyekaa
jela
mateso
ya mitaala
lakini
hukuchoka na wala
hukuwahi
kuwa na hasira.
leo
ardhi imekuita umeitika
leo
mwanao machoni umenitoka
hivi
ni nani tena shavuni atanishika
nani
huyo atakayekubali kuteseka
asije
sema amenichoka
mama…
hivi kweli ndo umeondoka.
ulikunja hata ngumi
Eti
kisa mimi…
Mama
ujue siamini
Nilikupenda
sana lakini
kumbe yupo alokupenda zaidi yangu mimi.
Ungekuwepo
mama ungenipenda zaidi yao
Ungekuwepo
mama ungejitoa kuliko wao
Ungekuwepo
mama usingekubali nichekwe nao.
Nakumbuka
mama
Hata
nilipo umwa
Ulilia
sana
Kifua
kilikujaa
Kando
yangu ulikaa
Hata
ukashinda njaa
Masaa
hadi masaa
Dear
mama
Hivi
kweli tutakutana
Au
ndo tutapishana
Hatutaonana
ilikuwa jana
mbona
ghafla sana
mara
ya mwisho kuwa_siliana
yaani
kama nakuona…
nilipokosea
ulinikemea
nilipoonewa
ulinitetea
niliporejea
ulinipokea
mama
leo upweke umeniachia….
vipi
moyo utatulia
Mwili
nguvu imeniishia
Ooo
huzuni imeniingia
Ujuwe
mama….
Sikuwahi
fikiria
Kuwa
siku itafikia
Safari
njiani utaishia
leo
mpweke nimebakia
Dear
mama
Nitawezaje
kuzoea
ili
hali uko mbali
nashindwa
kuelezea
ulivyo
mwema na mkweli
hukuwahi
kuniongopea
ulonitendea
ni mazuri
mahala
pema nakuombea
malaika
wa pepo akukubali
aweze
kukupokea
pasina
dosari.
Maoni