Shairi: Nakumbuka
Nakumbuka
Kila
Nikikumbuka yale matendo
Ukweli
na wako upendo
Mapigo
ya moyo yanaongeza mwendo
Nakumbuka
zile skendo
Nilipokupiga
kwa nyundo
Kisha
nikakusukuma kando.
Lakini
bado haukunichoka…
Nakumbuka…
Hata
kipindi nilipokuforce kuachika
Bado
hukuwa tayari kuondoka
Nilipo kuacha zaidi ya mwaka
bado
nyumbani hukutoka
nakumbuka
nilipo
rudi nilikukuta
tena
umejipata
ukawa
unanibembeleza
ukinituliza
huku
ukiniliwaza.
Ukiamini
nimebadilika
Nakumbuka
Hata
mwili wangu haukuwahi kuushika
Hata
uliponitaka
Nilidai
nimechoka
Usiku
ulipofika
Nilitoroka
Ila
bado hukunichoka..
Nakumbuka
Ulilia
kwa huruma
Huku
Ukionesha moyo unavyouma
Maneno
ya huzuni ukiyasema
Moyo
mkuki nauchoma.
Nakumbuka
Kwa
sauti ya kukwama
Pumzi
nzito ukihema…
Ukidai
nikuonee huruma
Daah
Sikukwelewa…
Maana
tayari nilikuwa nimelewa
Nakumbuka
Bila
huruma makofi na mateke nilikupiga
Huku
nikitoa sauti kali yakukuswaga…
Usiku
huo sikumbuki wapi ulilalaga
Nakumbuka
Unyama
nilio kufanyia
ile
siku ulipo nifumania
tena
kwenye kitanda tunacho lalia..
nakumbuka
sana uliumia
sana
ulilia..
lakini
bado hukuwahi kunichukia
nakumbuka
kosa
nifanye mimi
ajabu
msamaha uliomba wewe
furaha
kwakwo ilikuwa simulizi na visawe
niliyekufanya
mwewe mpigwa mawe
mwanamke
mvumilivu
tena
mkakamavu asiye na wivu
niliyekupaka
majivu
na
kukufunga nyavu…
nakumbuka
si
kwa mateso niliyokupa
viboko
nilivyokuchapa
nikakuita
kahaba
eti
mwizi wa kuiba
shingo
nilikukaba
pua
nikakuziba..
kiasi
cha kuleta msiba.
daaah
lakini
bado hukuchoka kunipenda…
tazama
leo
sina
maendeleo
sina
tegemeo
sina
upendeleo
wala
sina mwelekeo
naishia
kuulizwa yuko wapi mkeo
nakumbuka
ni
kama nakuona vile ukiwa jikoni
na
sahani mkononi
mwanamke
mcheshi
tena hodari wa mapishi
ulijua
kupambana ili tuishi
hukuwa
wa dharau wala kashikashi
nakumbuka ule wema wako
japo
kuwa sikuijuwa thamani yako
tazama
leo nalipa chozi lako
na
leo nashuhudia kifo chako
kwanini
uliniruhusu niuumize nafsi yako
kwanini
sikubakia upande wako
nakumbuka
ulinipenda
sana….
Uliumia
tulipogombana…
Ulifurahi
tulipokumbatiana
Ulipenda
kuona tukishirikiana.
Sasa
kwanini hayo yote sikuyaona..
Leo
peke yangu nang’ang’ana
Hakuna
anayeniona
Hata
majirani tumekosana
Sina
tena wa kuniamini
Wala
wa kunithamini
Kumbe
sikupendwa walinitamani
Laiti
ningelijuwa ya mbeleni
Nisingeruhusu
haya yajitokeze abadani
Kwa
maana yananinyima amani
Yananiumiza
rohoni.
Ona
sasa ndo hivyo unakwenda
Mwanamke
pekee uliyenipenda
Uliyepigana
kunilinda
Penzi
kubaya lisije enda
Kumbe
ubaya mwenyewe niliupanda
takukumbuka
Hivi
ndo kweli unaundoka
Au
naota….
Hivi
kweli unanitoka
Inamaa
tena sitakupata
Natamani
niweze hata kukushika
Natamani
tena uweze niita
Kwaheshima
niweze kuitika….
sasa
kwanini sikujuwa haya.
Maoni