Ushairi : Maumivu
Maumivu
Chriss..!
''Yes kili…!
Mambo vp brother…
''Fresh tu
Mbona
kinyonge sana
''Maisha tu
kaka…''
Yeah ni
kweli
but haupaswi kuwa katika hii hali.
Brooo kuna
vitu vinanichanganya ujue''
Vitu gani
hivyo
''Broo ni
kuhusu haya maisha.''
Chriss
unajuwa sikuelewi…… nambie tatizo nini?
''Broo
hivi unaweza kuyavulia nguo maji na
usiyaoge''
Hapana so
rahisi kiivyo.
(Kimya kidogo)
Chriss najuwa unachokifikiria
But ni
muhimu tukavumilia
Naelewa
magumu unayopitia
Naelewa ndio….
''Binafsi
nahisi nimekuwa jaribio la kila tatizo
Na kama ni
kapu basi ni lile kapu la taka za uozo
Sijakuelewa
nini unachomaanisha?
Broo sina
furaha…. Sina raha…
Na sijui ni
lini nitaondokana na huu ufukara….''
Chrisss….
Natambua…….
Natambua ni
kwa vipi ufukara unakera…
Ila fahamu
huwezi kuwa na furaha kama huna hela
Na hauwezi
kuwa na hela kama hauna nyenzo bora
Chrisss
naomba uutulize moyo
Naomba
usifikilie hayo
Kwa maana
mungu si mchoyo
Kama
binadamu tulivyo.
''Hapana kili
Ujuwe hili
linaniumiza sana akili.
Maana kila
nikifikili
Naishia
kuzalisha maswali
Kuwa hivi ni
kweli
Kwa hii
elimu yangu nilistahili
Kubebelea
tofari.''
Nooo chriss
usiseme hivyo…
Just ni
suala la muda tu…
Ni kweli
kazi ndo kila kitu
Najua kazi
nzuri hujenga heshima ya mtu
Na tena ni kipimo cha utu
lakini jambo
hili haliitaji haraka….
''Hapana kaka…
Kuna wakati
nachoka
Natamani
nirudi kule nilipotoka
Mwa mama
tumboni
Au kule
utotoni
Huenda
sitojuwa ya duniani.''
Sio rahisi
kiivyo
Na hata
hivyo hayo ni mawazo ya kitoto
Hivi ulisha
tembelea mahospitalini ukawaona walio na matatizo
Watu walio
elemewa na changamoto
Tena zaidi
yako
Mhhh hivi ulishafika mahakamani na polisi ukaona
watu wanavyokula msoto
Au omba omba
mtaani
Yatima wasio
na matumaini…
Ambao hawajui ni lini wataipata hauweni.
Please
chriss just calm down…
Naomba
uamini kuWa zamu yako ipo mbioni
Na kama si kesho basi tarajia siku za usoni.
''Kili unasema
nini
Ni mara
ngapi tunalala njaa bila chochote kitu tumboni
Mhhh ina
maana hauoni
Mhhhh ni
mwaka wa ngapi toka utoke chuoni
haya una
kazi gani….
Mhhh huoni….
Tutaishi
hivi hadi lini?
Eti kili..!
nijibu hili swali
tazama wengi
huko wanatanua
huku mimi na
wewe tunapigwa jua
haulioni
hili…''
chriss
kwahiyo
unatakaje…
tukavunje…
sema…
tukaibeeee
ili
tukamatwe
tupigwe mawe
tufe
au polisi
watushike
kisha
tufungwe
ni vipi
kuhusu ndoto zetu
au ndo
umesahau kila kitu
sasa nani
alaumiwe..
je wazazi au
serikali
au wewe…
sema….au
jamii nzima
kwa kosa la
kukubali
mitaala isiyo na ukweli
au tulaumu
wabunge matapeli
viongozi
wasio na maadili….
Eti sema
Chriss me
nafikiri
Tuendelee tu
na hii kazi ya tofari
Huwenda siku
moja itatupa utajiri
''Sawa kili
Nimekuelewa''
Basi vizuri kama umenielewa
Acha
tuendelee na kazi
na Kilimboka
Maoni