Shairi: Uhuru gani huu
Uhuru gani huu?
kama
maendeleo yatapimwa kwa mzani
unahisi
afrika itakuwa na majibu gani
najiuliza
hivi ni nani
alochimba shimo chini
kuzifukia
hizi mila na tamaduni
eti akaziita
ushetani.
Je ni sisi
watu wa gizani au wale watu wa motoni
Lakini kwanini tuliwaamini
Tukawakaribisha
kizimbani.
Kwanini
hatukuwapeleka utumwani…
Kwanini
hatukuwapeleka vitani.
Kwanini
tuliwaita wageni na si mashetani
Hivi
walijikuta akina nani.
Kwanini
hatukuwachapa viboko
Kwanini
hatukuwashika madako
Kwanini hatukuthamini
matambiko
Je haya ndo
yale mabadiliko
Na je ni
bora kuliko tutokako.
Kwanini iwe
ngumu kwa wenye ardhi
Kwanini iwe
vigumu kupata kazi
Au tupo
dunia ya maradhi
Dunia
isiyozingatia utamaduni wa mavazi.
Dunia
isiyotafuta radhi
Wala heshima
za wazazi
Dunia ya
mababu wasokuwa na hadhi
Eti miungu
ni upuuzi.
Dunia isiyo
jali usawa wala uwazi.
Mweupe mgeni ila mweusi mkimbizi
ardhi
iliyolithi mila za kipuuzi
mila ya
ushoga na usagaji.
Hivi ni nani
huyo mlogaji
Alotuloga
hadi akili
Leo
tumewasahau wapolaji
Wezi na
makatili
Leo tunaaita
wawekezaji
Leo
tunawaita watarii
Mbona mimi
siwaelewi.
Hawa si ndo
wale walobaka mabibi zetu
Kisha
wakawabebesha vitu
Wakawatembeza
kwenye misitu
Tena yenye
miba bila viatu
Ni viumbe
wenye roho za chatu
Ni binadamu
wasio na utu.
Ewe mwana wa
afrika
Kumekucha
sasa amka
Ewe mwana wa
nyika
Acheni sasa
kutawanyika
Maana wakati
umefika
Wa sisi sote
kubadilika.
Enyi kizazi
cha nyoka
Mlodanganywa
mmelaanika
Huu ndo
wakati wa sisi kuamka.
Hivi kwanini
tusingewafanya misukule
Kisha
tukawanyima shule
Badala ya
tatuu tukawachanja chale
Watakaoleta
ubishi tungewapiga mishale
au magobole
ili wakafie mbele.
hivi ni
kweli waafrika tumesahau
au ndo
kujisahaulisha
hivi ni
mkweli walio tudharau
leo
tunawaheshimisha
leo hii tunawaita
wadau
wakati wao
ndo walotufukaraisha.
mko wapi
mashujaa wa aunika na unika
wazalendo wa
kiafrika
mashujaa
mlopewa madaraka
sasa
mnakosaje mamlaka
wakati
mnajuwa fika
ni wapi
mlipotoka
maisha ya
utumwa na patashika.
Enyi
wasaliti wapenda noti
Mnakubalije
kutumika
Enyi walamba
nyayo washika goti
Ni lini
mtaja badilika
Mkaachana na
kuwa vizingiti
Mrudi nyumbani mnahitajika
Kwa pamoja
tujidhatiti
Ili afrika
iweze kubadilika.
Maana
kutumika unika tumechoka.
Tafadhari
rudini mlikotoka
Sasa
kizimbani mnahitajika.
Wanauwa
vipaji, kwa kutunyima kazi
Wameruhusu
ulaji, kuua vizazi
Wamekuwa
wanyonyaji , wamepandikiza mizizi
Hatuna
msemaji, afrika haina mkombozi.
Nauliza mko
wapi wazalendo wa kweli
mko wapi
mfano wa magufuli
Mko wapi
enyi majasiri
Mashujaa
msioogopa kabuli.
Hivi hadi
lini tutakubali
Kuwa
vibaraka wa nchi zao
Mbona
imekithili hii hali
Kupangiwa
bei za mazao
Tunaibiwa
rasilimali
Zinaenda
kwenye mataifa yao
Kwanini
serikali
Hamfanyi
kama wao.
Rushwa na
ufisadi
Sasa
mmegeuza ndo miradi
Pesa na
majumba ya ablodi
Afrika
kuipigisha hodi.
Na kilimboka
Maoni