Shairi : Mzalendo wa kweli
Naomba
kuuliza swali
Hivi ni yupi
mzalendo wa kweli
Kati ya raia
mpigwa na askari kwa kudai maisha mazuri
Au
polisi hodari mwenye kuitii serikali.
Hivi nani
mzalendo wa kweli
Kati ya raia
alojiajili
Au mgombea msema
kweli
Au masikini
alotumia nauli kujengea kabuli la tajiri
kisha
akaikosa safari ya kwenda kuichukua miili ya marehemu wake muimbili.
hivi kweli
taifa haliwezi kuwa na mashujaa wawili
kama ilivyo
kwa kitendawili na methali kuwa kipimo cha wenye akili.
Eti
shujaa gani
mponda mali
mzalendo
gani baili
unajihitaje
mtu wa watu wakati huna maadili
huna hekima
wala ujasiri
huna shuhuda
uliyemtoa mbali
akunadi
mbele ya umma ili wakukubali.
Mnaoomba
kula
mnauhakika
gani kama tumekula
au ndo
mnatuona mafala
tusiopenda
hela au siasa biashara.
aisee mnakosea sana
mnapoenda
msirudi
na mnapokuja
tena
eti
mnafungasha vizawadi.
mnajisahaulisha
mlichoahidi jana
kipindi
hatuna maisha hakuna anaye onekana
tukiwakumbusha tunaanza kudanganyana
mnachosha
afadhari yule wajana.
hivi kumbe
ndivyo mnavyo fanya
baada ya
kupata mlichotaka
haki zetu
mnatuminya
mnasahau
mliko toka.
mnafurahi
mmezikusanya
kodi za raia
walochoka
sasa hovyo
mwazitawanya
jasho la
mnyonge linatumika.
eti mnajiita
mzalendo
wakati
hamjui hata maana ya upendo
kutwa
biashara za magendo
mnatabasamu
sura kuficha matendo.
Haya sasa
viti ni vyenu
Mnaojiita
wazalendo wa jina
Haya sasa
wakati ni wenu
Kula starehe
za ujana
Mlizozikosa
kile kipindi chenu.
Kipindi
wazee wenu wakijichana
Wakati
walipoifanya taifa lenu
Kuwa shamba
la watwana.
Lini mtarudi
nyumbani
Lini
mtawakumbuka walio mashambani
Lini
mtashika mpini kupima ugumu wa ardhini
Lini mtakaa
barabarani kuuonja utamu wa juani
Lini mtapita
mashuleni au vyuoni Kuona wimbi la wakosa ajira mitaani.
Nauliza
lini mtaivaa
miwani ili mpate kujiona mlivyo mashetani.
Unajiitaje
mzalendo
wakati ni mwoga wa kupambana
unajiitaje
komando
wakati uoga
wako tunauona
utashindaje
kwa kishindo
wakati taifa
lako halina vijana wenye elimu za maana.
eti yupi
mwenye hasira
Yule
anayechoshwa na ufukara
au Yule
alochoka na kukaa jela.
ila naomba
waambie wavutaji wa sigara
‘’acheni
ufara…..’’
kuvutia
kwenye mihadhara
kwenye
mikusanyiko au daladala
waambie…
ila so kosa
lenu
bali ni wale
walio mbele yenu
maana hao
ndiyo wanaokuza vichwa vyenu
kujiona
wakishua kumbe waangukia pua
kujifanya
mnajuwa
kumbe
taratibu mnauliwa
mzalendo
gani wewe
unayejipenda
kuliko jilani yako
ufanye nini
tuelewe,
wakati
tunazijuwa tabia zako
kutwa kwenye
vijiwe,
ukisengenya
wenzako
msemaji
mwenyewe,
usiye na
hoja za mashiko.
na Kilimboka
Maoni