Shairi: Huoooooooo..!
Kaka hivi
ulisema utaoa lini?
Kwa kosa
gani?
Kwani kuoa
ni kosa?
''Hujui kama
ndoa ni kifungo''
So kweli
wewe ni muongo
Kama
utaniita mimi muongo je wenye ndoa utawaitaje
''Labda
wazugaji''
Hapo Utakuwa
na utani na wadangaji
''Kwaiyo ndoa
ni pango la kufichia maovu yao''
kaka
unautani na wenye ndoa zao
''Sio ndoa zao
sema wenye vifungo vyao''.
Ha ha ha
''Kaka''
Masikio yapo
wazi ongea
''Sawa,
nasikia siku hizi jamaa anatembea na remote controller''
Usiniambie,
ili iweje
''Umesahau''
Kaka
unajipenda kweli….
''Huooooooo''
aaa
nimekuelwa.
Kaka
''Mbwa wewe
nambie…''
Hivi nikiwa
chawa wao si nitanenepa
''Eee
utanenepa kama unakulaga nyumbani kwao…''
Kaka wivu
huo…
''Wivu kitu
gani mbwa wewe''
''Nawachukia
sana''
wananifurahisha mno
''Waliniunguzia
tv yangu ya chogo''
Walinilaza
gizani kama popo
''Ila wazuli
kwenye makato na malipo''
Aaa.. mimi siwakubali hata kidogo…
''Kwanza.. hivi ada yao ni shingapi''
Hata sijui
mainswitch yao iko wapi…
''Nasikia
meneja wao anatumia nishati wa jua''
Kwani solar na wao kipi bora
''bora jua….''
Maana giza
likifika mwezi unawaka.
''Afu Wao
wanazimika''
Ha ha ha ha
''Pumbavu zao''
Eti kaka
hivi mwanza ikikosa nyegezi itakuaje
''Labda
tuwaulize ubungo bila stend wanaishije''
Nahisi jibu
letu litakuwa mbezi…
''aisee sina
uhakika….''
Kaka
''hivi kuna kitakachabadirika''
Lini au huu
mwaka
''Kaka
sikuhizi kila kitu kimebadilika''
Mbona mimi
sioni
''Inamaana
siku hizi hauoni basi vaa miwani''
Kaka huo
utani
''Hivi kweli
hupaoni''
Sioni wapi
''Kaka
barabarani''
Kwani kuna
nini
''Inamaana
huoni… jinsi Ukimya ulivyotawala''
Acha
uendelee kututawala maana tulishakuwa
mafala ….Mbwa siye
''Afu kaka''
Nakusikia….
''Siku hizi sisikii kelele za magari wala
miungurumo kwanini''
Nikuulize
wewe fundi unayejisifu kwa udereva makini
''Au barabara
pana siku hizi…''
Nikuulize wewe
mpita njia
''Kaka au
umechukia kisa nilivyokuambia''
unatoa
majibu au unaulizia…
''Mhhh kwahiyo
hata honi hazipigi….''
Yaani ni
mwendo wa mnyefu… Yaani ni mwendo wa kimya kimya
''Hahaha
sikuhizi mji umekuwa na magari bubu…''
Kaka tatizo
so magari bubu tatizo ni njia
''Zimepanuka.''
Kwani greda
zimepita lini?
''Mbwa wewe…
kawaulize wapita kwa miguu.''
Na vipi
ukipita chocho
''Kaka huko
ndo usiseme kusha kuwa dimbwi… wakabaji wengi Kuna foleni hadi za bajaji..
Yaani chocho hazitamaniki Panya road wamejaa kila kona…. Nahisi hata huko ni
yale yale tu…''
Kwani askari
hawapo….
''Kaka polis
au patroo… naona hawausiki na huko''
kaka
''afu nimepata
kazi''
kazi gani
hiyo
''ni kazi ya
kuchimba mitaro ya maji taka''
unakoelekea
utaanza kufukua mitalo ya mavi taka
''bora
tunaofukuwa kuliko wanaofumua bomba za
maji taka''
Sijakuelewa
hapo…
''Kaka mimi
huko simo''…
Huoooooooooo
''Duuu hawa
nao kwa kujisikia''
Yaani saa
hii ndo wanaturudishia
''wanakoelekea
nitahama mtaa''
Uhamie wapi
''Dodoma''
Kwakumuogopa
obama
''Au Yule
binti osama''
Kaka huko
jua halizami hovyo
''Kwakuwa huko
ni mwezini au , mbwa wewe…….''
Kaka nina
swali
''Ila usiulize
kitendawili''
Hivi
kunamaana gani nikisema hakombi mboga bila kulamba bakuli.
''Kabla
sijakujibu''
Kwanza
kamuulize mpishi eti kati ya kidole na bakuli kipi hulambwa kwa ulimi.
''Ujuwe sio
pilipili…''
Utawashwa
wewe….. hadi ukome
''Ujuwe sio
mimi…''
''Hatari hiyo
mboga haichagui ugali''
Umekubali
eeeee
''Hapana labda
wali hauchagui kachumbali''
So kweli
''Ni mboga ndo
haichagui pilipili''
Ila mimi
nahisi nyama choma
''Ndo
inaendana na wali''
Hapana
''Inaendana na
ugali''
Basi labda
kachumbali….
''Wewe unasema
nini…''
aaaaa hamna…
''Mbwa wewe''
Ila kuna
wakati huo wako vizuri
''Aaa mimi
siwakubali''
Kwa kukata
''Wamefanyaje...?''
Aaaa
umekataaaaaaaa.
''Hawa nao
hawana kazi za kufanya….''
Badala ya
kukata mauno
''Wanakata
waya''
Kaka hivi
waya ukikatikia ndani umeme utawaka
kweli.
''Nahisi
transfoma itafeli.''
Kaka hivi
kwenu wapishi wanaruhusiwa kulamba mwiko
''Kwani nyie
mnaruhusiwa kula kwa mwiko.''
Ni kosa kwa
mila zetu
''Sisi ni
dhambi kwa destuli yetu''
Kaka mimi
nimechoka
''Umechoka
nini..''
Nimechoka
kufukuza mende
''Sasa wewe
unaishije na mende''
Ndo nyumba
za kupanga zilivyo tafanyaje
''Hauna dawa
uwapulizie''
Kaka
nimechoka kuwauwa
''Kaka
huchoshwi na vifo vya mende''
Nichoswe
vipi wakati sitaki hata niwaone
''Kaka mimi
ujue nina huruma sana''
Hata
nikimkuta mende nyumbani ameanguka chali
''Aisee lazima
nimgeuze''
Sipendi
atembelee mgongo muda mrefu coz nahisi kama anaumia vile..
''Acha ushamba
wewe..''
Ungemuacha
vilevile tena ungemkanyaga hadi afe….
''Kaka kuwa na
huruma wewe…''
Nao ni
viumbe…
''Sio kwa
mende hawa sasa.''
Aisee kwani
ni mende gani hao
''Si wale
wakianguka chali hawawezi kujigeuza''
Kwani ni
wale wakubwa au wadogo
''Kaka maswali
gani hayo wewe juwa ni mende''
Basi chunga
sana wasije wakawa wale mende wa maradhi.
''Ukaanza
kuzunguka huku na kule ukitafuta tiba''
Kama ni hivyo
mwakani najenga nyumba nzuri na ya kisasa
''Hayo ndo
mambo.''
Kaka jenga
nyumba yako hao mende sio…
''kaka unataka
kusema kuwa wenye nyumba hawaishi na mende''
Kaka
tueshimiane nimeoa juzi ujue
''Kaka nina
habari mpya''
Ni mpya
kweli .
''Nasikia
sikuhizi vibogoyo wanang’ata nyama…''
Hiyo kuukuu
leta nyingine
''Nasikia siku
hizi wanaume wananyonya vidole''
Unashangaa
nini ?
''Kwani
wanawake hawanyonyi vidole''
Kaka vidole
si wananyonya watoto….
''Sio watoto
bali watoto wadogo.''
Una mpya
nyingine
''Kaka nasikia
siku hizi takataka hawamwagii ndani wanamwagia jalalani''
Unasema nini
wewe?
''Sasa ulitaka
wamwagie wapi''
Mbwa wewe…
''Wamwagie
chooni''
Labda chooni
kwako
''kaka
usichukie nauliza tu…''
mbwa wewe.
Maoni